Tangakumekuchablog
Tanga,
WAFANYABIASHARA wenye maduka jijini Tanga, wametishia kufunga maduka yao ikiwa
Kikosi Cha Zima Moto na Uokozi kitaendelea kuwabughuzi wafanyabiasha hao kwa
kuwataka kuweka kifaa maalumu cha kuzimia moto(Fire Extingsher).
Wakizungumza katika mkutano wa
wafanyabiashara ulioitishwa kufuatia kikosi hicho kupita madukani kuwataka
kuweka kifaa hicho na kufunga maduka, wamesema endapo wataendelea watafunga
maduka yao na kufanya mgomo.
Wamedai sheria hiyo ni kandamizi na hivyo kukitaka
kikosi hicho kuacha mara moja kuwabughuzi wafanyabiasha na badala yake
kuangalia changamoto zinazowakabili.
Wamesema kikosi hicho kiko na
changamoto nyingi zikiwemo uhaba wa magari na maji ya kuzimia moto na kuchelewa kufika
kwa wakati maeneo ya matukio .
Tangakumekuchablog ilifanya jitihada za kuzungumza na kamanda wa kikosi cha Zima Moto Tanga, kuzungumzia malalamiko hayo lakini ilishindikana na kuelezwa uongozi uko katika kikao.
Mwisho
No comments:
Post a Comment