Sunday, May 17, 2015

WATU WAWILI WAUWAWA KATIKA SHAMBULIO LA BOMU

2 wauawa katika shambulizi la bomu Kabul

l.
Watu wawili wameripotiwa kufa na wengine wengi kujeruhiwa baada ya mlipuko kutokea kwenye uwanja wa kimataifa wa ndege katika mji mkuu wa Afganistan Kabul.
Walioshuhudia wanasema kuwa mlipuaji wa kujitolea mhanga alikuwa amelenga wanajeshi wa kimataifa nje ya lango kuu la uwanja huo wa ndege.
Haijabainika iwapo walikwepa shambulizi hilo au la.
Lango hilo hutumika na maafisa wa kijeshi wa kigeni pekee yao.
Mtu aliyeshuhudia alilitaja shambulizi hilo kuwa la kujitoa mhanga.
Msemaji wa polisi nchini humo amaiambia BBC kuwa shambulizi hilo lilifanyika karibu na afisi za halmashauri za safari za ndege nchini humo zilizoko nje ya uwanja wa ndege.
Shambulizi hilo linafanyika siku tatu baada ya mwanamgambo mmoja kuwaua watu 14 wakiwemo raia 9 wa kigeni mjini humo.
Hutopitwa na habari inayonifikia na niko tayari kukutumia muda wowote kupitia hapa hapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment