Tangakumekuchablog
Tanga,
MWENYEKITI wa kamati ya Afya Baraza la Madiwani halmashauri ya jiji la Tanga,
Sele Boss Mustafa, amewataka wauguzi kuzingatia maadili ya kazi zao na kuacha
kutoa siri za wagonjwa.
Akizungumza katika kongamano la
shamrashamra kuelekea maadhimishoya siku ya wauguzi Duniani jana, Mustafa
alisema kuna baadhi ya wauguzi wamekuwa wakivunja maadili ya kazi zao kwa kutoa
siri za wagonjwa.
Alisema kufanya hivyo ni makosa na
kutaka kuwepo kwa sheria kali kwa watu ambao wako na tabia kama hiyo na kudai
kuwa mgonjwa huwa katika wakati mgumu mtaani mara baada ya kutoka hospitali.
“Kwa vile leo nimepata nafasi ya
kuzungumza nanyi basi niwaase wale ambao wako na tabia ya kutoa siri za
wagonjwa kuacha kufanya hivyo-----ni jambo baya na halifai kufanywa” alisema
Mustafa
“Ili kuweza kudhibiti tabia hii ni
lazima kuwepo kwa sheria ambazo zitamuwajibisha atakaetoa siri za mgonjwa kwani
kuna baadhi ya wagonjwa hawatoi ushirikiano mzuri kwa wauguzi kwa hofu ya siri
yake kutangazwa” alisema
Amewataka wauguzi hao kuwa na
mshikamano na upendo pamoja na kuipenda kazi yao mbali ya changamoto nyingi
ambazo wamekuwa wakikumbana nazo na kusema kuwa mchango wao kwa jamii
unatambulika.
Akizungumz akatika kongamano hilo,
Muuguzi wa jiji, Ester Kimweri amewataka wauguzi kuwa karibu na wagonjwa pamoja
na kuwapa maneno mazuri kwa kuwafariji.
Alisema kuwa na utamaduni huo
kutawafanya wagonjwa kupata faraja wakati wote wanapokuwepo hospitali jambo
ambalo pia linaweza kuwa sababu ya kupona maradhi wanayokabiliana nayo.
“Wauguzi wenzangu tuendelee na
mshikamano wetu kama kawaida pamoja na kutoa maneno mazuri kwa wagonjwa ili
kuwapa faraja----huu ndio utamaduni wetu hasa sisi tuliopo hapa” alisema
Kimweri
Amewataka wauguzi hao kufanya kazi
kwa bidii kwani mbali ya kazi pia wako na fungu mbele ya Mungu kwani huduma zao
ni njema na hivyo kuwataka kuendeleza kasi ya utoaji wa huduma.
Mwisho
No comments:
Post a Comment