Tanga, WAANDISHI
wa habari Tanga, wametakiwa kuvitumia vyombo vyao vya upashaji habari
kuielimisha jamii katika zoezi la uchukuaji wa alama na upigaji picha ili kila
mmoja kuweza kupata kitambulisho cha Taifa.
Akizungumza na waandishi wa habari
ofisini kwake jana, Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Abdalla Lutavi, alisema vyombo vya
habari viko na nafasi kubwa ya kulifanikisha zoezi la vitambulisho vya Taifa.
Alisema jamii kubwa ya watu hasa wa
vijijini bado haina uelewa mpana wa kuwa
na vitambulisho vya Taifa na hivyo kuvitaka kuzipa nafasi kubwa ya kutoa elimu ya kwenda kujisajili na kuweza kupata
kitambulisho.
“Zoezi hili bila vyombo vya habari
linaweza kuiwanyima makundi ya watu haki ya kuwa na kitambulisho cha
Taifa----nawaombeni sana kuelimisha jamii umuhimu wa vitambulisho” alisema
Lutavi na kuongeza
“Hebu sasa vyombo vya habari
kujikita maeneo ya vijijini kwani kuna makundi ya kijamii bado hayana uelewa wa
kuwa na kitambulisho cha taifa----ili kuweza kulifanikisha hili ni ninyi
waandishi wa habari kuandika sana juu ya kitambulisho cha taifa” alisema
Alisema waandishi wengi wa habari
wamekuwa waking’ang’ania habari za mjini na kusahau makundi ya jamii za
vijijini na hivyo kukosa fursa nyingi za kihabari pamoja mambo mengine ya kijamii.
Akizungumza katika mkutano huo,
Afisa habari mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) Rose Mdami,
aliwataka Watanzania kujitokeza kwa wingi katika kujisajili kwani vitambulisho
hivyo viko na umuhimu mkubwa katika Nyanja mbalimbali za kijamii.
Alisema kuacha kufanya hivyo mtu
ataweza kupoteza haki na fursa nyingi zikiwemo za utambulisho wa utaifa na
hivyo kuwataka kujitokeza na kutoa vielelezo sahihi.
“Nawaomba Watanzania wenzangu
kujitokeza kwa wingi katrika zoezi la upigaji picha na uchukuliwaji wa alama
pamoja na kutoa taarifa sahihi----hii itasaidia mustakbali mzima wa zoezi la
vitambulisho” alisema Mdami
Aliwataka kuzitumilia vyema siku
zilizotolewa za upigaji picha na alama na kihakikisha kila mmoja ameweza
kulifanya jambo hilo muhimu binafsi na kwa Taifa.
| ||||
No comments:
Post a Comment