Friday, February 3, 2017

KOCHA WA QUEEN FAIR PLAYA YA TANGA, KIPIGO CHA MABAO 3 AMWACHIA MUNGU

Tangakumekuchablog, Tanga

Tanga, KOCHA wa timu ya wanawake JKT Queen  inayoshiriki ligi kuu Tanzania Bara, Robarts Ngolija, amesema siri ya ushindi mnono walioupata wa mabao 3, 1  kutoka Queen Fair ya Playa ya Tanga ni umakini wa wachezaji wake.
Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mpambano huo, kocha huyo alisema wachezaji wake walikuwa makini na kujitambua wanachokifanya uwanjani.
Alisema walitambua kuwa Fair Play ni timu kali yenye wachezaji mahiri hivyo wachezaji wake waliuanza mchezo huo kwa umakini na kuwasoma kila dakika ilivyokuwa ikienda.
“Ushindi ule ni umakini wa wachezaji wangu kwani wakati tunakuja kucheza tulitambua kuwa tunaenda kupambana na timu ngumu, niliwaona wachezaji wangu wanauanza mpira kwa kasi bila mimi kuwapa maelekezo hayo” alisema Ngolija na kuongeza
“Nafikiri wakati wanaingia uwanjani wao wenyewe waliambizana namna ya mchezo wauanze, na ndio maana magoli yalingia kama mvua na kupelekea bao la pili wakajifunga” alisema
Aliwapongeza wachezaji wake kwa uchezaji waliouonyesha na kuwataka ushindi huo kuwa chachu na endelevu ili kufanya vizuri katika mechi zilizoko mbele yao.
Kwa upande wake kocha msaidizi wa Queen Fair Play ya Tanga, Mansour Alawi, alisema haamini kilichotokea uwanjani lakini yote anamuachia Mungu.
Alisema hakuna mchezaji wa kumlaumu na kuona kila mmoja licheza vizuri zaidi ya mwenzake na kusema kulikuwa na jinamizi ambalo limepita hivyo kusema anamwachia Mungu.
“Kwa matokeo ya leo namuachia Mungu kwani sina wa kumlaumu ila niseme kuwa kuna jinamizi limepuliza wachezaji wangu mabao matatu kama mvua sio kitu ambacho tumekizoea” alisema Alawi
Aliwataka wachezaji wake kusahau matokeo hayo badala yake kufanya mazoezi kwa bidii yakiwemo ya kukimbia pamoja na kuogelea baharini ili kuwa na pumzi za kukimbia uwanjani kwa dakika 90 bila kuchoka.
                                          Mwisho





,Kiungo wa JKT Queen, Merry Masatu, akimdhibiti beki wa Queen Fair Play ya Tanga wakati wa ligi kuu ya Wanawake  Tanzania Bara uwanja wa Mkwakwani jana, JKT Queen ilishinda kwa mabao 3  ,  1.

 Wachezaji wa Queen Fair Play ya Tanga wakigombea mpira na wachezaji wa JKT Queen wakati wa mchezo ligi kuu ya Wanawake Tanzania Bara uwanja wa Mkwakwani jana , JKT walishinda kwa mabao 3, 1.

No comments:

Post a Comment