Sunday, January 11, 2015

MIRIPUKO INAYODAIWA KUTUMIWA NA WAHALIFU YAKAMATWA, KOROGWE TANGA

BASI LA KLM EXPRESS LAKAMATWA LIKIDAIWA  KUSAFIRISHA SHEHENA YA MILIPUKO ENEO LA KOROGWE, TANGA


 Milipuko hiyo baada ya kukamatwa mchana huu ikiwa ndani ya boksi
Kuna shehena kubwa ya milipuko ya hatari inayotumika kutengenezea  Mabomu ya Kuvulia samaki na kutengenezea milipuko ya kupasulia miamba migumu imekamatwa eneo la Korogwe mchana huu wakati wa Jeshi la Polisi walipokamata Basi la KLM EXP lenye usajili wa namba T491 ARB kwa ajili ya Ukaguzi. Milipuko hiyo ambayo imesafirishwa kwa njia ambayo sio sahihi kutokana na hatari yake ya kuwa kulikuwa na abiria na kama Basi Lingetingishika zaidi Ingeweza Kulipuka .

 Askari wa Jeshi la Polisi Katika Kituo cha Korogwe akikagua Milipuko hiyo


 Basi hili limetumika kusafirisha Milipuko hiyo


Taarifa zaidi itakuijia hivi punde endelea kutufuatilia
Kumekuchablog iko kwa ajili yako na lolote linalojiri itakuhabarisha

No comments:

Post a Comment