Kumekucha blog
Pemba,VIJANA mji wa Wete Wilaya ya
Kaskazini Pemba wameitaka Serikali kuruhusu biashara ya kubeba abiria maarufu kama (bodaboda) ili kuondokana na wimbi
la vijana wasio na kazi na kuacha kujingiza katika magenge ya wavuta bangi na wabwiaji wa unga.
Wakizungumza
na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti jana, vijana hao wamelalamika
kuzuiwa kubeba abiria kwa madai kuwa
hakuna sheria inayoruhusu
kufanya hivyo.
Walisema
kuruhusiwa kubeba abiria kwa kutumia pikipiki ingelileta mabadiliko makubwa kwa
vijana mjini humo baada ya walio wengi kutokuwa na kazi na badala yake wamekuwa
wakikaa katika baraza za kahawa na kupiga soga.
“Vijana
wengi hawana ajira rasmi na wala hakuna kazi ya kufanya ukapata kipato ukaweza
kujiendesha maisha yako---tumekuwa tukiwaona vijana wenzetu katika maeneo Bara
wakibeba abiria na kujiuliza kwa nini na sie tusiwe kama wao” alisema Salim Ali
“Huku kwetu
hakuna daladala za kuingia mashamba na katikati ya mji hivyo kuwepo kwa
bodaboda ingekuwa msaada kwa jamii na sisi vijana kujikwamua na maisha na
kuepuka kukaa katika baraza za kahawa na kupiga soga lisilo na maana” alisema
Kwa upande
wake mkazi wa Chanjaani Shehia ya Gando, Shaban Nassour, amewataka vijana
kujituma kwa kufanya kazi kwa bidii na kuacha kuilalamikia Serikali ili kuwapatia kazi.
Aliwambia
kuwa Serikali kazi yake ni kuharakisha palipo na maendeleo na kutoa msukumo na
hivyo kuwataka kuonyesha dhamira ya kweli katika kujikomboa na umasikini katika
maeneo yao kwa kufanya kazi kwa bidii.
Alisema kuna
baadhi ya vijana wamekuwa wakilalamika kukosa kazi ilhali hawaonyeshi dalili
zozote za kujituma na badala yake wamekuwa wakiilalamikia Serikali kutowapa
kazi.
“Wakati
mwengine baadhi ya vijana wenzangu huniona kama mtu nilietumwa na kuwa na
maslahi----mimi ni mwanaharakati wa maendeleo kwa vijana wenzangu na ndio maana
naumia sana kuwaona wakiwa hawana kazi na kujikalia katika magenge na baraza za
soga” alisema Nassour
Aliwataka
kufanya kazi kwa bidii na Serikali kuwaona na kuweza kuwasaidia katika mipango
yao ya kujikomboa na umasikini na kuwa msaada kwa wengine ambao wamekuwa
wakikata tamaa ya maisha.
Mwisho
No comments:
Post a Comment