Monday, February 9, 2015

MVUTANO WA MAITI DAR WALETA KIZAAZAA

Hii ni Hekaheka ya leo Feb 9 inatokea Dar; inahusu msiba ulioleta mvutano.

The wind blows out candleJumatatu ya leo February 09  inatokea Dar kuhusu msiba ulioleta mvutano uliopelekea maiti izuiliwe kuzikwa baada ya mume  wa marehemu kutaka msiba ufanyike nyumbani kwake Kigoma, huku ndugu upande wa mwanamke wakipingana na wazo hilo na kutaka mazishi yafanyike Dar.
Ndugu mmoja wa marehemu amesema kuwa ndugu yao alikuwa anaumwa ugonjwa ambao hawakuujua, mume wake ndio alikuwa karibu naye akimuuguza mpaka alipofariki kitu ambacho kilifanya ndugu kuhusiisha kifo hicho hicho na imani za kishirikina.
Ndugu hao wamesema kuwa wanachotaka ni kushiriki mazishi ya ndugu yao lakini mume huyo alikataa ndugu yoyote kushiriki kwenye jambo lolote kwenye msiba huo ikapelekea suala hilo kufikishwa Mahakamani lakini baadae walikaa na kukubaliana kufanya mazishi Dar.
Mume huyo amesema kuwa mke wake alipokuwa anaumwa hakupata msaada wowote kutoka kwa ndugu japokuwa walikuwa na taarifa juu ya kuumwa kwa mke wake.

No comments:

Post a Comment