Tuesday, March 21, 2017

FAIDA YA TANGO KATIKA MWILI WA BINADAMU

Tumia Tango Kwa faida zifuatazo

Leo katika makala hii afya tujifunze  faida za Tango katika miili yetu, ikiwa watu wengi tunakula bila kujua faida zake katika maisha ya kila siku. Hivyo nakusihi uambatane nami mwanzo mpaka mwisho wa makala haya kwani naamini utakochokisoma hapa kitakwenda kukusaidia.

Zifuatazo ndizo faida za tango:
1. Tango ni chanzo kizuri cha vitamin B. Ambayo husaidia kwa kiwango kikubwa katika kusafisha figo. Na kuondoa sumu zote zilizomo mwilini.

2. Tango husaidia kuongeza maji katika mwili wa mwanadamu, kwani asilimia 95 ya tango ni maji, huku tukizingatia ya kwamba asilimia 75 ya mwili wa mwanadamu ni maji,  ambapo maji hayo ni chanzo kikuu cha usafirishaji wa chakula na damu katika mwili wa mwanadamu. Hivyo unashauriwa utumie kwa wingi tunda hili.

3. Tango pia hutumika kwenye matunzo ya ngozi/urembo ambapo tunda hili lina kiwango kikubwa cha silicon na sulfur ambazo husaidia ukuwaji wa nywele.

4. Tango lina virutubisho kama lariciresinol, pinoresinol na secoisalariciresinol ambavyo kulingana na tafiti mbali mbali za magonjwa ya kansa husaidia kupunguza aina mbali mbali za kansa hasa kansa ya matiti.

5. Kwa wale ambao wana matatizo ya kinywa hasa harafu wataalamu wanasema ya kwamba tango husaidia kuondoa harufu mbaya kinywani.

7.Tango husaidia wagonjwa wa kisukarikwani tango lina hormone ambayo huhitajika kwenye chembechembe za kongosho (pancreatic cells) ilikuweza kutengeneza insulin ambayo husaidia kudhibiti kiwango cha sukari kwenye mwili hivyo kuwasaidia wagonjwa wa kisukari. Pia watafiti wamegundua kuwa kuna kirutubisho kiitwacho sterol kilichopo kwenye tango ambacho husaidia kupunguza mafuta kwenye mishipa ya damu.

8. Kutokana na maji na virutubisho vilivyopo kwenye tango, tunda hili husaidia kupunguza homa pale inapopanda.

Cha msingi na cha kuzingatia ni kwamba kula matunda mara kwa mara kwani yana saidia sana katika afya. Endelea kutembelea muugwana blog kwa makala kama hizi.
MGBLOG

No comments:

Post a Comment