Klabu ya Manchester City,
imeshitakiwa na chama cha soka cha nchini England FA, kwa kushindwa
kuwathibiti wachezaji wake waliomzonga mwamuzi Michael Oliver, katika
mchezo dhidi ya Liverpool.Oliver alitoa adhabu ya penati baada ya kuona Gary Clichy, amemfanyia madhambi Roberto Frimino, katika eneo la hatari, na mkwaju huo wa penati ukapigwa na James Milner aliyeukwamisha wavuni.
City wanatakiwa mpaka siku ya Alhamis kuwa wamepeleka utetezi wao kwa chama hicho cha soka cha England.
No comments:
Post a Comment