Friday, March 10, 2017

JAFO AMPA MKANDARASI STENDI MPYA YA MABASI KOROGWE SIKU 22 AKAMILISHE UJENZI



KOROGWE, NAIBU Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Suleiman Jafo, amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Korogwe, Robarts Gabriel, kuhakikisha Mkandarasi ujenzi wa stendi mpya ya Kilole anakamilisha mwishoni mwa mwezi huu vyenginevyo akatwe pesa na kunyimwa tenda Wilayani humo.
Akizungumza wakati wa ukaguzi wa stendi hiyo inayojengwa na kampuni ya Namis Coperate  Contractor ambayo iliomba kuongezewa muda, Jafo alisema lazima ujenzi huo ukamilike ndani ya mwezi huu.
Alisema stendi hiyo ilitakiwa kuanza kutumika kwa mabasi yaendayo Mikoani na Wilayani hivyo kutaka ikamilike kabla ya mwezi huu kuisha.
“Mkuu wa wilaya nakuagiza stendi hii kama haitakamilika mwisho wa mwezi huu mkandarasi akatwe pesa na kunyima tenda zote za halmashauri yako” alisema Jafo.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Korogwe, Robarts Gabriel aliwataka wafanyabiashara na wasafirishaji kuitumia stendi hiyo mara baada kukamilka kwa uchumi wa Wilaya hiyo.
Alisema stendi hiyo ambayo mabasi yote yaendayo Mikoani na Wilayani yatakuwa yakiingia hivyo kuwataka wafanyabiashara kuwekeza katika miradi mbalimbali ya kibiashara.
Nae Mbunge wa Korogwe Vijijini (CCM) Stivin Ngonyani, aliwataka wajasiriamali wadogowadogo wakiwemo wa kazi za mikono wataweza kujitangaza na kuuza bidhaa zao tofauti na stendi ya zamani ambayo ilikuwa finyu.
Alisema kukamilika kwa stendi hiyo kutaweza kuinua kipato cha wajasiriamali wadogowadogo hivyo kuwataka kujiimarisha katika kazi zao.
‘Ujio wa stendi mpya ni neema kwa wajasiriamali wadogowadogo hasa wa kazi za mikono kwani mabasi yote yaendayo na yatokayo mikoani yataingia stendi hiyo ambayo itakuwa ya kisasa” alisema Majimarefu
Aliwataka wananchi wa Korogwe kuipokea stendi hiyo kwa kubuni biashara ambazo zitaweza kuwabadilisha kimaisha kwa kuenua vipato vyao.






No comments:

Post a Comment