Friday, March 31, 2017

MWILI WA KIM JONG WAWASILI KOREA KASKAZINI

Bwana Kim ni ndugu wa kambo wa kiongozi wa Korea KaskaziniRaia wa Malaysia wakaribishwa nyumbaniMwili wa Kim Jong-nam, ndugu wa kambo wa kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un, umewasili nchini Korea Kaskazini.
Korea Kaskazini ilikuwa imeomba kupewa mwili huo lakini haikuwa imesema ulikuwa ni wa nani.
Mwili huo ulitolewa kwa Korea Kaskazini kama sehemu ya makubaliano ambapo raia 9 wa Malaysia, waliizuiwa kuondoka Korea Kaskazini waliwasili nyumbani.
Nchi hizo mbili zimekuwa kwenyr mzozo wa kidiplomasia kufuatia mauaji ya Kim, kwenye uwanja wa Kuala Lumpur mwezi uliopita.
Nchi hizo mbili zimekuwa kwenyr mzozo wa kidiplomasia kufuatia mauaji ya Kim, kwenye uwanja wa Kuala Lumpur mwezi uliopita.
Kila nchi ilikuwa imewapiga marugufuku raia wa nchi nyingine kuondoka.
Raia watatu wa Korea Kaskazini wameruhusiwa kuondoka malaysia, kwa mujibu wa mkuu wa polisi wa nchi hiyo.
Korea Kaskazini inashukiwa pakubwa kuhusika kwenye kifo cha  Kim, kwa kutumia kemikali akiwa uwanja wa Kuala Lumpur.
BBC

No comments:

Post a Comment