Friday, March 10, 2017

MWANAMKE MWENYE UZITO KILO 500 APUNGUA HADI KILO 100 BAADA YA MATIBABU, INDIA

Eman Ahmed Abd El Aty baada ya kufanyiwa upasuajiMwanamke wa Misri anayeaminiwa kuwa mwenye uzito wa juu zaidi duniani akiwa na kilo 500, amefanyiwa upasuaji wa kupunguza unene chini India.
Msemaji wa hospitali ya Saifee mjini Mumbai amesema kuwa Eman Ahmed Abd El Aty, mwenye umri wa miaka 36, amepungua kilo 100 baada ya upasuaji.
" Tunajaribu kumuwezesha kuwa mwenye nguvu za mwili kuweza kusafiri nyumbani Misri haraka iwezekanavyo," ilieleza taarifa ya hospitali.
Familia yake ilisema kuwa hajawahi kuondoka nyumbani kwao kwa miaka 25 hadi siku aliposafirishwa hadi India mwezi Januari kwa ndege.

No comments:

Post a Comment