Friday, March 24, 2017

RAIS WA ZAMANI MISRI, HOSNI MUBARAK AACHIWA HURU

Aliyekuwa rais wa Misri Hosni Mubaraka ameachiliwa huru baada ya kuhudumia kifungo cha miaka kadhaaAliyekuwa rais wa Misri Hosni Mubarak ameripotiwa kuachiliwa huru baada ya kuhudumia miaka jela kufuatia maandamano yaliomng'atuwa mamlakani 2011.
 Mubarak alikuwa akizuiliwa katika hospitali ya kijeshi mjini Cairo, lakini wakili wake aliiambia BBC kwamba sasa ameruhusiwa kurudi nyumbani kwake mjini humo.
Aliagizwa kuachiliwa huru mapema mwezi huu baada ya mahakama ya rufaa kumuondolea makosa ya kuwaua waandamanaji wakati wa maandamano dhidi yake 2011.

No comments:

Post a Comment