Monday, March 6, 2017

POLISI, TRA YANASA BIDHAA ZA MAGENDO,TANGA



Tanga, JESHI la polisi, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kushirikiana na vyombo vyengine vya ulinzi vimekamata shehena za mali ya magendo katika bandari bubu ya Kigombe.
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ghala la kuhifadhia mali jana, Menaja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Tanga, Swalehe Byarugaba, alisema shehena hizo ni pamoja na mchele, sukari, madumu ya mafuta na viberiti kutoka nje vyenye thamani zaidi ya milioni 73.
Alisema kwa wiki nzima wamekuwa wakifanya doria hasa vyakati za usiku katika bandari bubu ya Kigombe na sehemu nyengine ambazo wamekuwa wakipokea taarifa za ushushaji wa mali za magendo.
“Kama munavyoona humu hizi zote ni mali za magendo ambazo tumekuwa tukifanya doria katika bandari zetu na kufanikiwa kukamata na zote zikiwa ni kutoka nje” alisema Byarugaba
Alisema katika mali hizo manahoza wa vyombo wamevitekeleza vyombo vyao na wengine kufanikiwa kuwakamata na kuwachia vyombo vya usalama kwa hatua za kisheria.
Akizungumza kwenye uonyeshaji wa mali hizo za magendo, kamanda wa polisi Tanga, Benedickti Wakulyamba, alisema kikosi chake kwa kushirikia na vyombo vyengine vya ulinzi wamekuwa wakifanya doria usiku na mchana bandarini na mpakani horohoro.
Alisema kuna baadhi ya washukiwa wa mali za magendo wamekuw wakihojiwa na wengine kufuatilia na kutoa onyo kwa wasafirishaji wa mali za magendo kuwa wametangaza vita.
Alisema doria hiyo itakuwa endelevu usiku na mchana hivyo kufuatilia nyendo za watu ambao wamekuwa wakiwahisi kujihusisha na biashara ya haramu ikiwemo mali za magendo.
“Natangaza vita kwa wasafirishaji wa mali za magwendo na wapitishaji wa madawa ya kulevya kuwa hakuna mlango wakupitishia, na yoyote ambaye atajaribu cha mtema kuni atakiona” alisema Wakulyamba
Alisema jeshi hilo linawashikilia watuhumiwa wa madawa ya kulevya ikiwemo mihadarati na wasafirishaji wa mali za megendo na uchunguzi ukikamilika watafikishwa mahakamani.
                                               







 Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Tanga, Swalehe Byarugaba (kushoto) na Kaimu Meneja msaidizi Forodha Tanga, Jumbe Magoti wakiangalia nembo ya moja ya mifuko 1,308 ya mchele kutoka nje iliyokamatwa katika bandari bubu ya Kigombe wakati wa operesheni iliyofanywa wiki nzima kwa kushirikiana na jeshi la polisi, TRA, wavuvi na vyombo vya usalama na kukamata bidhaa mbalimbali zenye thamani zaidi ya shilingi milioni 73.

No comments:

Post a Comment