Friday, March 31, 2017

SPACE X YARUSHA TENA ROKETI KWA MARA YA PILI ANGA ZA JUU

Satelite ya SES-10 iliyosafirishwa na Falcon 9 iliundwa nchini Uingereza na UfaransaFalcon 9 ikiwa tayari kupaa kutoka kituo cha Kennedy Space CenterKampuni ya kuunda roketi za wanasayansi wa anga za juu ya SpaceX iliyo na makao yake huko Carlifonia, Marekania, imefanikiwa kurusha tena roketi yake kwa kutumia moja ya roketi zake aina ya Falcon 9.
Awamu ya kwanza ya roketi hiyo ambayo ilitumika tena miezi 11 iliyopita, ilitumiwa kutuma satellite ya mawasilano kuenda kwa mzingo wa dunia, kutoka kituo cha safari za anga za juu cha Kennedy Space Center.
Hiyo ni hatua kubwa wa kampuni ya SpaceX katika majaribio ya kutumia roketi mara ya pili.

No comments:

Post a Comment