Friday, March 17, 2017

MADEREVA WALEVI TAIWAN WAKOMESHWA

TaiwanHapa Tanzania, Uganda , Rwanda na hata Burundi  na Kenya utaona mabango makubwa yamewekwa kando ya barabara kuonya madereva kuto endesha magari wakiwa wamelewa .
Mabango hayo mbali na kukutishia kwamba unaweza kufariki kutokana na ajali, pia yanaonya kwamba ukipatikana utatozwa faini kubwa kama njia ya kukutia adabu kwa kosa la kuendesha gari ukiwa mlevi.
Lakini nchini Taiwan mambo ni tofauti kabisa.
Dereva yeyote anayepatikana na kosa la kuendesha gari akiwa mlevi , anakamatwa na kupelekwa kwenda kufanya kazi katika chumba cha kuhifahdi maiti.
Mkuu wa mashtaka katika jimbo la Taitung huko Taiwan, ameiambia BBC kwamba madereva wanaopatikana na kosa la kuendesha gari wakiwa wamelewa wanapewa kazi maalum ya kusafisha meza za kuwa pasulia maiti. Na pia wanatakina kuosha na kusafisha kabisa friji za kuwekea maiti.

No comments:

Post a Comment