Sunday, January 11, 2015

WATOTO HAWAKUAMINI MASIKIO YAO KUSIKIA ELIMU YA UZAZI

Watoto hawa hawakuamini wanachokisikia kuhusu elimu ya uzazi, tazama video hapa

download (1)
Kulingana na ukuaji wa teknolojia watoto wadogo wamekuwa na uelewa wa mambo mengi, japo sio vizuri wakajua kila kitu wakiwa na umri mdogo,  je kama mzazi ulishawahi kukaa na mtoto wako  ukajaribu kumdadisi kama anauelewa wa kujua jinsi mtoto anavyopatikana?
Hiyo ni elimu kubwa kidogo na hata watu wazima kuna mazingira ambayo sio rahisi wakakaa kuyazungumzia, kutoka Marekani team ya cut.com imebuni kipindi cha mazungumzo na watoto, kinaitwa “Birds and the Bees Talk”  ambacho wazazi huzungumza ukweli  na watoto wao ishu mbalimbali.
Swali ambalo limeulizwa kwa watoto hawa ni kuhusu kupima utashi wao wanaelewa nini kuhusu namna mtoto anavyopatikana?
Baadhi ya watoto walijibu kwamba Mungu alituma mtoto kwenye tumbo la mama ili waweze kuzaliwa, na wengine wakajibu wanavyohisi ni sawa, shida ikawa pale walipoelezwa ukweli!
Icheki video na picha zao wakati wa mjadala huo mtu wangu.
chuyenay5_PKKY
parents-give-their-kids-the-sex-chat
Video_Teaser (1)

Hautopitwa na stori yoyote inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia, kumekuchablog

No comments:

Post a Comment