Wednesday, March 9, 2016

AFISA MFAWIDHI SUMATRA TANGA AWAJIA JUU WENYE MABASI



 Afisa Mfawidhi Sumatra Tanga, Walukani Luhamba, akizungumza na waandishi wa habari wa Tanga, kuzungumzia wamiliki wa mabasi ya abiri na daladala kuzingatia bei elekezi baada ya nishati ya mafuta kushuka bei.
Luhamba aslisema ni jukumu la kila mmiliki wa gari la abiria kushusha nauli kwa kutambua kuwa mafuta yameteremka bei hivyo hakuna sababu yoyote ya kung'ang'ania nauli za zamani.
Alisema Ofisi yake itafanya ukaguzi mara moja na yoyote ambaye atabainika kung'ang'ania nauli za zamani atazuiliwa leseni yake ya biashara.







No comments:

Post a Comment