Monday, March 14, 2016

MAJIMAREFU AHIMIZA KAYA KUJIUNGA NA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII



Tangakumekuchablog
Korogwe, MBUNGE wa jimbo la Korogwe Vijijini (CCM), Stivin Ngonyani maarufu Majimarefu, amewataka wananchi jimboni humo kujiunga na mifuko ya Hifadhi ya Jamii ili kupata matibabu bure.
Akizungumza katika mikutano yake ya kuwashukuru wananchi kwa kumchagua kwa mara ya pili kuwa Mbunge wao kata ya Lewa na Hale, Majimarefu alisema kila kaya ihakikishe imejiunga na mifuko ya Hifadhi ya Jamii na kuweza kufaidika na huduma ya matibabu bure kwa gharama kidogo.
Alisema gharama ya matibabu na madawa madukani iko juu ambapo watu wengi hawana uwezo wa kumudu kutokana na vipato vyao hivyo ni wajibu wa kila mtu kutambua kuwa kujiunga na mifuko ya Jamii inaweza kuondoa ukali wa maisha  mmoja ndani ya familia wakati  akiugua.
“Ndugu zangu wananchi wapiga kura wangu tutambue kuwa kuna mifuko ya hifadhi ya jamii ambayo ukijiunga unapata matibabu bure  pamoja na wenza si zaidi ya wanne” alisema Majimarefu na kuongeza
“Lakini niseme kufanikisha hili nitazungumza na hiyo mifuko ya jamii kuja kwenu kuwapa elimu kwanza ili mutambue umuhimu wa kujiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii” alisema
Akizungumzia umuhimu wa kujiunga na vikundi vya Ujasiriamali, Majmarefu aliwataka wanawake na vijana kuunda vikundi ili kufaika na mikopo yenye riba nafuu na kuweza kutunisha mifuko yao.
Alisema vikundi viko na faida nyingi ikiwemo kupata mikopo na misaada hivyo kuwataka makundi hayo kufanya hivyo ambavyo pia itavutia watu wengine jambo ambalo litapunguza umasikini na watu wasio na kazi.
“Watu wengi hawatambui kuwa vikundi vya ujasiriamali ndivyo vinavyowatoa kimaisha, ukweli ni kuwa kujiunga kunafaida nyingi ikiwemo mikopo katika taasissi za fedha na hata Serikali” alisema Mbunge huyo
Aliwataka watu kufanya kazi na kujuwa wajibu wake pamoja na kuzitumia rasilimali zilizoko ikiwemo kilimo cha chai na mbogamboga na matunda na kusema kuwa masoko yapo.
Alisema wafanyabiashara wako huru kutafuta masoko likiwemo  la pamoja la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) hivyo kuwataka kulitumilia kwani litawawezesha kutangaza biashara zao na kubadilishana uzoefu.
                                                    Mwisho







No comments:

Post a Comment