Monday, March 14, 2016

AFRICAN SPORTS YAITUMBUA JIPU MBEYA CITY

 Timu ya African Sports ya Tanga, jana imewakonga washabiki wake kwa kuifunga Mbeya City magoli 2 bila na kurejesha matumaini ya kubakia ligi kuu Tanzania Bara.
Timu hiyo ilionyesha dalili toka dakika ya kwanza ya mchezo baada ya kuonyesha kandanda safi huku washambuliaji wake , Hassan Materema, Ali Ramadhani na Hamza Khamis wakiliiandama lango la Mbeya City.
Washabili waliwashangilia kwa nguvu wachezaji na kila walipokuwa wakikaribia lango la Mbeya City walitoa burudani ya nguvu na kusaidia kuibuka kwa magoli mawili.

  Washabiki wa African Sports ya Tanga, wakiishangilia kwa nguvu timu yao wakati wa mchezo ligi kuu Tanzania Bara uwanja wa Mkwakwani jana.



Mshambuliaji wa African Sports, Fadhili Kizenga, akijaribu kutafuta mbinu ya kumtoka beki wa Mbeya City, Joseph Mahunzi wakati wa mchezo ligi kuu Tanzania Bara Uwanja wa Mkwakwani jana.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa Tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment