Wednesday, March 16, 2016

MAKONDA AWATAKA WAKUU WA IDARA NDANI YA MASAA 24 KUWASILISHA RIPOTI ZA IDARA ZAO

Mkuu wa mkoa Paul Makonda kaanza kazi Dar… maagizo ya kwanza ni haya

Jana March 15 2015 Rais John Pombe  Magufuli aliwaapisha wakuu wapya wa mikoa 26 ya Tanzania bara na kuwaagiza kutekeleza wajibu wao bila kuwa na hofu yoyote kutoka kwa watu ikiwa ni pamoja na kuwashughulikia watendaji wote watakaoonekana kuwa wazembe kwenye sekta zao, leo Marh 16 2016 ndio mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda amekabidhiwa rasmi ofisi ili kuuongoza mkoa wake.
Licha ya hayo yote Makonda alipata time ya kufahamiana na baadhi ya watendaji katika ofisi yake, na hapohapo akatoa agizo la kuwataka wakuu wote wa idara kumfikishia ripoti zao ikiwa ni pamoja na changamoto zinazowakabili ndani ya saa 24.
Tumeingia kwenye awamu nyingine ya kuongoza mkoa unaojulikana kama Dar es salaam lakini ukiwa na wilaya tano, sio kazi ndogo, natakiwa kuwa na wilaya mpya mbili ambazo kwa mara ya kwanza napata nafasi ya kuona namna gani zikianzishwa
wananchi wanashida ya maji, barabara, matibabu, migogoro ya ardhi nakadharika, lakini waliamini kumpa majukumu Rais Magufuli ili awatatulie changamoto hizo‘ ;-Paul Makonda
Rais huyo kaamua kwa Dar es salaam amkabidhi majukumu hayo Makonda ili aifanye hiyo kazi, Sasa ninawataka wakuu wote wa idara ndani ya saa 24 mnipatie ripoti ya kila idara mliyonayo‘ ;-Paul Makonda
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa Tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment