Thursday, March 24, 2016

CHAMA CHA WANASHERIA TANZANIA (TAMLA) YALIA NA UKATA WA PESA



Tangakumekuchablog
Tanga, CHAMA Cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA), kimesema bajeti ndogo inawakwaza kuweza kukabiliana na changamoto za kuwalinda watoto kupata haki zao.
Akizungumza katika kongamno la siku moja la maofisa polisi, mahakimu na maofisa ustawi wa jamii jana, Mjumbe wa baraza Tawla Makao Makuu, benadela Hassan, alisema ufinyu huo unashindwa kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.
Alisema upungufu wa maofisa Ustawi wa jamii ni chanzo cha haki za watoto na wanawake kupindishwa hivyo kuishauri Serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii na watoto na wazee kuongeza maofisa ustawi wa jamii kila kata.
“Bajeti ndogo imekuwa kikwazo cha Tawla kufanya kazi zake zikiwemo za kuhakikisha ulinzi wa watoto na wanawake kupata haki zao, hatuna maofisa ustawi wa jamii wa kutosha” alisema Benadela
Alisema ili kuweza kuzilinda haki hizo za watoto na wanawake ni Serikali kuhakikisha inaweka maofisa maendeleo jamii ili kuweza kusimamia haki hizo tofauti na ilivyo sasa ambapo watoto hawatendewi haki.
Kwa upande wake, Hakimu mkazi Mfawidhi Wilaya Tanga, Azaiza Lutalla, alisema wazazi wanashindwa kuwachapa watoto wao kwa hofu ya kupelekwa katika madawati ya jinsia.
Alisema kuna baadhi ya wazazi wanawaogopa watoto kuwachapa hivyo kuyataka madawati kutoa elimu majumbani namna ya kutoa adhabu kwa watoto wanapokosea.
“Kuna wazazi wanawaogopa kuwachapa watoto kwa hofu ya kuwapeleka katika madawati ya kijinsia, je hapa inakaaje kwani kwa hofu hiyo watoto hawataweza kuwa na maadili mema ya Kitanzania” alisema Lutalla
Alisema ili kuweza kujua haki za wazazi na watoto hasa wanawake ni wajibu wa madawati ya kijinsia kuhakikisha inatoa elimu majumbani na kuweza kutokomeza unyanyasaji kwa wanawake na watoto majumbani.
                                         Mwisho



 Wakili wa Serikali, Jeniffer Kaaya, akizungumza kwenye kongamano la Chama Cha Wanasheria Wanawake Tanzania (Tawla) lililofanyika jana Tanga na kuwashirikisha makundi mbalimbali pamoja na dawati la Jinsia na Watoto Tanga kupitia ofisi ya kamanda wa polisi Mkoa jana.

Picha ya pamoja viongozi wa Chama Cha Wanasheria Wanawake Tanzania (Tamla) baada ya kumalizika kongamano la siku moja kujadili Changamoto zinawakabili wanasheria nchi.

No comments:

Post a Comment