Tuesday, March 22, 2016

MAJIMAREFU AWAPA SOMO WAKULIMA



Tangakumekuchablog
Korogwe, MBUNGE wa jimbo la Korogwe Vijijini (CCM), Stivin Ngonyani maarufu Majimarefu,amewataka wananchi kujiandaa na mvua zinazotarajiwa kunyesha kwa kutayarisha mashamba na kuacha kuuza kwa wageni.
Akizungumza katika mikutano ya hadhara jana kata ya Kizera na Foroforo, Majmarefu aliwataka wananchi kuacha kuuza mashamba na badala yake kujiandaa na mvua zinazotarajiwa kunyesha hivi karibuni.
Alisema kuna taarifa za wageni kuwarubuni wakulima kuuza mashamba yao kwa bei rahisi kwa kitisho cha mvua kuacha kunyesha hivyo kuwambia kuwa waache kwani mvua zipo na karibuni zitanyesha.
“Ndugu zangu wazee wangu na wajomba zangu nimepata taarifa za kuwepo kwa watu kutoka nje ya hapa kuja kuwarubuni ili muwauzie mashamba yenu, nawaomba chonde chonde musithubutu kwani mutakuja jutia” alisema Majimarefu na kuongeza
“Wanakuja na pesa zao za uchwara kisha kuwaingiza katika umasikini na njaa, mimi kama mbunge wenu sitakubali na ninalifuatilia kwa ukaribu taarifa hizi kwani zimenisononesha” alisema
Akizungumzia upatikanaji wa pembejeo za kilimo na uwepo wa maofisa ugani mashambani, Mbunge huyo alisema atahakikisha Serikali inawapeleka maofisa hao na kuwa karibu na wakulima.
Alisema mara nyingi wakulima wanashindwa kupata mavuno mazuri baada ya kukosa wataalamu wa kilimo hivyo msimu huu wa kilimo atahakikisha maofisa hao wanakuwa karibu na wakulima.
“Kila mtu anajua kuwa maofisa kilimo kwa baadhi ya maeneo hawafiki waliko wakulima, ndio maana hukosa mavuno na balaa la njaa huwakumba” alisema
Aliwataka wakulima kutayarisha mashamba yao na kujiandaa na kilimo kwa madai kuwa mvua ziko karibuni kunyesha hivyo katika kufanikisha kilimo hicho ofisi yake ya mbunge itasaidia upatikanaji wa mbegu.



 Mlima mkubwa uliopo kata ya Kizara Korogwe Vijijini kama ilinavyoonekana
 Moja ya majengo kata ya Kizara Korogwe Vijijini katika muonekano wake






 Mbunge wa Korogwe Vijijini (CCM), Stivin Ngonyani, maarufu Majimarefu, akizungumza na wananchi kata ya Foroforo kwenye mkutano wa hadhara kuwashukuru kwa kumchagua kwa mara nyengine tena jana.
  Wananchi kata ya Foroforo Korogwe Tanga, wakimsikiliza Mbunge wa Korogwe Vijijini, Stivin Ngonyani, maarufu Majimarefu wakati wa mkutano wa hadhara kutoa shukurani kwa kumchagua tena kuwa Mbunge wao.


 Vijana wa Kata ya Magoma Korogwe jimbo la Korogwe Vijijini wakipozi na Gari la Mbunge wao Prosefa Majimarefu jana wakati alipoenda kuwasalimu na kuwashukuru kwa kumchagua tena kuwa mbunge wao na kusikiliza kero zinazowakabili.


No comments:

Post a Comment