Saturday, April 30, 2016

AFRICAN SPORTS YAIPELEKA KATIKA TUNDU LA SINDANO COASTAL UNION, YAIBAMIZA BAO 1 BILA

 Timu ya African Sports imevunja ngebe za kaka zao Coastal Union baada ya kuifunga bao moja pekee dakika 28 kwa mshambuliaji wake hatari , Ali Ali.
 Bao hilo la mapema lililodumu hadi kipenga cha mwisho kimewaweka katika wakati mgumu Coastal Union na wako katika tundu la shindani la kubaki ligi kuu Tanzania Bara msimu ujao.



 Mshambuliaji wa Coastal Union, Miraj Adam akimtoka beki wa African Sports ,Issa Shaban wakati wa mchezo ligi kuu Tanzania Bara uliochezwa uwanja wa Mkwakwani leo




 , Beki wa Coastal Union Hamis Mbwana akimtoka mshambuliaji wa African Sports, Mussa Chambega wakati wa mchezo ligi kuu Tanzania Bara uwanja wa Mkwakwani Leo.
  Polisi wa kutuliza ghasia (FFU) wakiimarisha ulinzi baada ya washabiki kutaka kufanya fujo baada ya refarii kumpa kadi nyekundu mchezaji wa African Sports, Ali Ali dakika ya 28,wakati wa mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara kati ya Coastal Union na African Sports zote za Tanga  uliochezwa uwanja wa Mkwakwani leo.

No comments:

Post a Comment