Sunday, April 17, 2016

KOCHA JANGALU ACHEKELEA USHINDI MFULULIZO



Tangakumekuchablogspot.com
Tanga, KOCHA Mkuu wa Coastal Union ya Tanga, Ali Jangalu, amesema ushindi walioupata wa bao moja  kwa Ruvu JKT, ni sawa na kuwapeleka nusu fainali ya mashindano hivyo kila timu iliyoko mbele yao ni ushindi tu.
Jangalu alisema hayo mara baada ya kuisha kwa mchezo wake na Ruvu JKT uwanja wa Mkwakwani jana, na kusema morali wa ushindi waliupata wakati walipotoa kipigo kizito Simba wiki moja iliyopita.
Alisema wachezaji wake wameingiwa na hamasa ya ushindi na wamekuwa wakicheza kwa kuelewana na kudhamiria kila mchezo ulio mbele yao  kupambana kupata ushindi kuepuukana na janga la kushika daraja.
“Mchezo ulikuwa mgumu kwani wapinzani wetu niseme ukweli walicheza vizuri zaidi ya sisi lakini nasi tulipambana vya kutosha hadi dakika ya mwisho, ushindi huu ni sawa na kuingia nusu fainali ya ligi hii ukifungwa mechi moja umekula mweleka” alisema Jangalu na kuongeza
“Lakini pia ushindi huu umekuwa mtamu zaidi kwa ndugu zetu African Sports pale tutakapokutana nao, nadhani mechi hiyo ni sawa na fainali ya kombe la dunia” alisema
Jangalu alisema kwa ushindi huo mfululizo wamedhamiria kupambana kufa na kupona na kuwambia wachezaji wake kuwa sasa hakuna kuremba mipira bali na mashuti tu langoni mwa wapinzani toka dakika ya kwanza hadi dakika za nyingeza za mwamuzi.
Kwa upande wake, Kocha wa Ruvu JKT, Abdalla Kibadeni, alisema Coastal Uniona wako na bahati na kusema kuwa wachezaji wake walicheza zaidi ya wao hivyo pointi tatu kuwaangukia wao.
Alisema walicheza zaidi ya wao lakini uwanja uliokuwa na maji uliwasaidia kupata bao kwa kutumia uzoefu hivyo na kusema kuwa safari bado ni ndefu na wanarudi kujipanga upya.
Alisema wachezaji wake walicheza vizuri na hakuna hata  mmoja alieonyesha kucheza chini ya kiwango lakini bahati ya Mungu ikimuangukia mja hauwezi kuipangua.
“Sisi tulicheza vizuri zaidi yao lakini niseme kuwa bahati ya mja Mungu akimruzuku hakuna wa kuipangua na leo hii ndio imetokea kwa Coastal, uzoefu wa uwanja uliokuwa na maji pia umewasaidia” alisema Kibadeni
Alisema ligi ilipofikia bado wako na nafasi ya kusonga mbele mbali ya upinzani mkubwa kwa timu ambazo zinafunga na pointi na kusema kuwa watapambana hadi mchezo wa mwisho.
                                                  Mwisho



Washabiki wa Coastal Union ya Tanga, wakiishangilia timu yao wakati wa mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara  na  Ruvu JKT Uwanja wa  Mkwakwani jana, Coastal Union ilishinda kwa bao 1.




  Kocha wa Coastal Union ya Tanga, Ali Jangalu, akimuangalia mchezaji wake, Yussuf Chuma akichuana na mabeki wa Ruvu JKT, wakati wa mchezo ligi kuu Tanzania Bara uwanja wa Mkwakwani jana. Coastal Union ilishinda kwa bao 1.
Mchezaji wa Coastal Union, Chidebere Abdisalam, na mchezaji wa Ruvu JKT Renatus  Morris, wakifukuzia mpira wakati wa mchezo ligi kuu Tanzania Bara uwanja wa Mkwakwani jana , Coastal Union ilishinda kwa bao 1.

No comments:

Post a Comment