Thursday, April 21, 2016

ARSANAL WENGER KIBURI

Baada ya Wenger kupata taarifa kuwa mashabiki wa Arsenal hawatokuja uwanjani leo April 21 2016

April 21 2016 hii inaweza ikawa siku ambayo kocha wa klabu ya Arsenal ya Uingereza Arsene Wenger hatoisahau kama kweli itatokea kama ambavyo inaripotiwa na mitandao, kuwa mashabiki wa Arsenal wamepanga kutokwenda uwanjani leo April 21 2016 katika mchezo kati ya Arsenal dhidi ya West Brom ili kushinikiza Wenger aondoke.
Baada ya stori hizo kuenea mitandaoni waandishi wa habari walimpata kocha wa Arsenal Arsene Wenger azungumzie kuhusu hiyo stori, kama mashabiki wakigoma kweli kuja uwanjani katika mechi ya leo April 21 2016 ataendelekea kusalia Arsenal au ataondoka?
Arsene Wenger, Manager of Arsenal.
Arsene Wenger
“Siwezi kuzungumzia suala la mimi kuondoka Arsenal tena, bado na mkataba na Arsenal na nina hueshimu, kuhusu mashabiki kutokuja uwanjani kila mmoja ana maamuzi yake na tiketi yake ya msimu, mtazamo wa watu kupenda kujaji, ni tabia ambayo tunalazimika kuishi nayo lakini ipo ndani ya uwezo wetu kuibadili” >>> Wenger
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa Tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment