Monday, April 25, 2016

KOCHA JANGALU USHINDI WA YANGA AMWACHIA MUNGU




Tangakumekuchablog
Tanga, KOCHA wa Coastal Union, Ali Jangalu, amesema anakubali mamuzi ya mwamuzi ya kupokea kipigo cha mabao mawili kutoka kwa Yanga, lakini amedai hakuna ubishi timu yake imehujumiwa.
Alisema hayo jana  mara baada ya dakika 105  ya mchezo wake na Yanga uwanja wa Mkwakwani, na kudai kuwa bao la Hamis Tambwe halikuwa sahihi na badala yake alikuwa ameotoea.
Alisema timu yake ilicheza zaidi ya Yanga lakini bahati haikuwa yao hivyo maamuzi ya mwamuzi ndio sahihi na hana la kusema hivyo anawaachia washabiki walivyoliona goli la pili .
“Uzuri wa mchezo huu ulikuwa unaonyeshwa moja kwa moja, mimi nikilalamika kama bao lile halikuwa sahihi nitaonekana kama naminyana, kwa hivyo nawaachia wao waseme” alisema Jangalu na kuongeza
“Hata kama tuko katika janga la kushuka daraja lakini timu yangu ilicheza vizuri zaidi ya wao, niseme kuwa hatuna bahati ya ushindi kila siku sie tunacheza vizuri lakini tunafungwa” alisema
Alisema kama mwamuzi asingelivunja bambano hilo mchezo ungelikuwa wao na kuwapongeza wachezaji wake kwa kuonyesha kandanda safi ya kuvutia na kuwataka kusahau ya mwamuzi na kuangalia michezo iliyoko mbele yao ligi kuu.
Alisema kila mchezaji alicheza kwa kujituma na kujua wajibu wake uwanjani na kwa matokeo hayo anawapongeza na kuongeza morali uwanjani ili michezo iliyoko mbele yao waweze kushinda.
Kwa upande wake mshambuliaji wa Coastal , Ahmed Shiboli alisema Yanga waliwashika kila idara na kusema kuwa walikuwa na bahati ambayo wanatakiwa kuishukuru kwani wangeondoka kwa aibu.
Alisema kwa mchezo walivyouanza toka dakika ya kwanza ya mchezo ni dhahiri walipaswa kuondoka na pointi tatu  ambapo walipeleka mashambulizi mengi langoni mwao
Alisema beki ya Yanga waliisumbua na baadhi ya mashuti kuokolewa na kipa wao ambao upande wa kiungo Abdulhalim Humood aliisumbua safu ya ushambuliaji ya Yanga.
                                                   Mwisho


No comments:

Post a Comment