Thursday, April 21, 2016

WATOTO WAWILI WAFAMAJI KWENYE SHIMO LA SHOO , TANGA



Tangakumekuchablog
Tanga, WATOTO wawili wakazi wa Kange Kasera Tanga , Antony Godfrey (3) na Emmanuel Aidan (4)  wamekufa maji baada ya kutumbukia katika shomo la choo lililopo nje ya nymba ya jirani yao.
Tukio hilo limetokea jana saa 4 asubuhi na kuthibitishwa na kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Leonard Poul  na kusema kuwa polisi inafanya uchunguzi wa tukio hilo ili kama kulikuwa na uvunjaji wa sheria ya ujenzi sheria ziweze kuchukuliwa.
Akizungumza tukio hilo baba mzazi wa Antony, Godfrey Komba, alisema alipata taarifa za mtoto wake kufa maji akiwa njiani akitokea kazini jambo ambalo lilimchanganya kwani asubuhi yake aliwaacha wakiwa na afya njema.
Alisema alipatwa na  mshtuko baada ya kupata taarifa za tukio hilo na wakati alipokuwa akikaribia nyumbani kwake alimkuta mke wake, Flora Vicent akilia na majirani wakiwa wamekusanyika kwa wingi.
“Hapa jirani kuna shimo la choo liko mbele ya mlango wake na lilikuwa limejaa maji mengi na lilikuwa halijafunikwa, watoto wangu na wajirani wamekuwa wakicheza na mara nyingi nilikuwa nikiwambia wasicheze karibu na lile shimo” alisema komba na kuongeza
“Shimo hili limejaa maji kufuatia mvua kubwa ilionyesha juzi kwa siku mbili mfululizo, tukio limeshatokea sina la kusema na kwa sasa ndio tunashughulikia mazishi” alisema
Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti msibani hapo, wakzi wengi wameitaka mipango miji kuweka sheria ya ujenzi hasa wa mashimo ya choo.
Walisema kuna baadhi ya wajenzi wamekuwa wakichimba mashimo ya vyoo kisha kuyatekeleza na kuwa hatari kwa watoto na mifugo.
                                              Mwisho


 Wakazi wa Kange Kasera Tanga, wakimfariji Flora Vicent, mama wa mtoto , Antony Godfrey Komba, aliekufa baada ya kutumbukia katika shimo la choo lililokuwa limejaa maji karibu na nyumba yao jana.



No comments:

Post a Comment