Saturday, April 23, 2016

SHIBOLI AJIPA MOYO



Tangakumekuchablog
Tanga, MSHAMBULIAJI wa Coastal Union ya Tanga, Ahmed Shiboli, ameiambia Yanga kuwa wasitarajie kuchukua pointi tatu Tanga, bali watarajie kipigo kama walichokitoa kwa Simba wiki mbili zilizopita.
Akizungumza mara baada ya kufanya mazoezi Uwanja wa Mkwakwani  leo, Shiboli alisema timu hiyo imeiva na iko tayari kwa mchezo huo ambao watapigana kufa na kupona ili pointi tatu zibaki Tanga.
Alisema kwa sasa timu hiyo iko kwa kusubiri mchezo huo kwani wameibva na hakuna mapungufu kuanzia mlinda mlango washambuliaji na kumezingatia mbinu walizopewa na wakufunzi wao.
“Kwanza mimi mwenyewe nakuhakikishia nitafunga goli, kuna jambo nimeongeza wakati wa  mazoezi, ningekuwambia lakini sitakui kiwe hadharani kwani mabeki wa Yanga wataniandama wakati wa mechi” alisema Shiboli na kuongeza
“Tunmekuwa tukifanya mazoezi kwa siku mara mbili mfululizo na tumekuwa kambini na muda mwingi tumekuwa tukipewa mbinu za kuimaliza Yanga, nikuhakikishie hatoki mtu kesho” alisema
Alisema anatambua kuwa Yanga itakuwa ikicheza kama Mbogo aliejeruhiwa kwa kipigo cha Tunisia ila kwetu itakuwa ikitupa morali kwani tukiweza kumfunga goli la mapema atanyongea.
Kwa upande wake Msemaji wa Coastal Union, Osker Assenga, ameiambia Mwanaspoti kuwa wachezaji wameiva na wako tayari kwa mpambano huo ambao alidai ushindi ni lazima.
Alisema hakuna sababu ya kupoteza mchezo huo ambao ni muhimu na utakuwa umewajenga katika kinyang’anyiro cha kubaki ligi kuu msimu ujao wa ligi ambapo amesema ligi iko lala salama.
“Niseme kuwa wachezaji wameiva na wanasubiri siku ya kesho kuingia uwanjani, hatuna majeruhi wala mgonjwa, tunwaomba wakazi wa Tanga kuja kuishangilia timu hiyo na kuibuka na ushindi” alisema Assenga
Ameiambia Yanga kuwa wasitarajie kuibuka na ushindi Mkwakwani kesho kwani watatoa kipigo kama ilichokitoa kwa Simba wiki mbilizi zilizopita kwa kutumia uzoefu kwa uwanja na nyumbani.
                                               Mwisho

No comments:

Post a Comment