Monday, April 18, 2016

WAHAMIAJI 400 KUTOKA SOMALIA WAZAMA BAHARINI

Wahamiaji 400 kutoka Somalia wazama baharini

Maelfu ya wahamiaji kutoka Afrika na Mashariki ya Kati wamekuwa wakijaribu kufika Ulaya
Wahamiaji karibu 400, wengi wao kutoka Somalia, wanahofiwa kuzama katika bahari ya Mediterranean wakijaribu kuelekea bara Ulaya.

Taarifa kutoka Misri zinasema wahamiaji hao walikuwa wakitumia boti nne kusafiri.

Jamaa za baadhi ya wahamiaji hao wamesema baadhi ya wahamiaji waliokolewa na kikosi cha wana maji kutoka Ugiriki na kupelekwa katika jiji la  Grees..

Balozi wa Somalia nchini Misri amethibitisha kisa hicho lakini akasema bado wanatafuta maelezo zaidi kujua chanzo hicho na eneo la safari walioanzia.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa Tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment