Sunday, April 17, 2016

KATIBU MKUU UTUMISHI WA UMMA AWAPA SOMO WATUMISHI WA AFYA BOMBO TANGA



Tangakumekuchablog
Tanga, KATIBU Mkuu, Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma, Lauren Ndumbaro, amewataka madaktari na wauguzi hospitali ya Rufaa ya Bombo Tanga, kufuata maadili ya kazi ikiwa na pamoja na kutunza siri za wagonjwa.
Akizungumza mara baada ya kukabidhi kifaa maalumu cha matangazo cha kutolea taarifa za Afya kwa wagonja na wafanyakazi hospitalini hapo kilichotolewa na Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) juzi, Ndumbaro alisema kuna baadhi ya watumishi hukiuka maadili ya kazi zao.
Alisema kuna tabia iliyojengeka kwa wadaktari na wauguzi kutoa siri za wagonjwa na kusahau maalidili ya kazi hivyo kutaka kuachwa tabia hiyo ambayo imekuwa ikiwadhalilisha wagonjwa katika jamii.
“Leo nimekuja hapa katika uzinduzi wa kifaa cha matangazo kwa wagonjwa na wafanyakazi hospitali kilichotolewa kupitia mradi wa ndugu zetu wa Ujerumani, kupitia hadhara hii niwatake kuzingatia maadili ya kazi zenu” alisema Ndumbaro na kuongeza
“Kuna baadhi ya wauguzi na madakari hutoa siri z wagonjwa jambo ambalo ni kinyume na maadili ya utumishi, ili kuikomesha tabia hii kila mmoja awe askari wa mwenzake kupitia kitengo hiki cha kupokea matangazo” alisema
Aliwataka watumishi hao kufanya kazi kwa bidii na kuondosha malalamiko kwa wananchi juu ya huduma zitolewazo katika hospitali na vituo vya afya vya Serkali nchini.
Kwa upande wake, Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) Godwin Kabalika, amesema shirika hilo limekuwa likisaidia hospitali mbalimbali kuboresha mifumo yake ikiwemo ya mawasiliano pampja na utunzaji wa kumbukumbu za fedha.
Alisema mfumo huo wa mawasiliano kwa wagonjwa na wafanyakazi utakuwa ukitoa taarifa mbalimbali za afya na upatikanaji wa huduma sehemu husika ikiwa na pamoja upokeaji wa malalamiko kwa wateja.
“Msaada huu ni moja ya miradi ya shirika la Ujerumani katika kusaidia hospitali hapa nchini kuboresha mifumo yake ya utunzaji kumbukumbu na mawasiliano na shughuli nyengine za kijamii katika hospitali” aliksema Kabalika
Aliwataka wahusika wa kifaa hicho cha mawasiliano kukitunza na kuwa msaada kwa wafanyakazi na wagonjwa kwa kupeana taarifa pamoja na upokeaji wa taarifa za malalamiko na nyenginezo zihusianazo na Afya.
                                                 Mwisho



Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma, Dr, Laurent Ndumbaro (katikati)  akipatiwa maelezo na mganga Mfawidhi hospitali ya Rufaa ya Bombo, Dr, Jumanne Karia (kulia) wakati alipotembelea mara baada ya kukabidhi kifaa cha kutolea taarifa za wagonjwa na wafanyakazi hospitali (Paplic Adress System) kupitia Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ)  kushoto ni, Mkurugenzi wa Ukuzaji Maadili Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma, Mathew Kirama.


  Dakatari bingwa wa watoto hospitali ya Rufaa ya Bombo, Dr,  Murtaza Rasheed (kulia) , akimpatia maelezo juu ya magonjwa ya watoto wakati alipotembelea hospitali hapo mara baada ya makabidhiano ya kifaa maalumu cha kutolea taarifa za wagonjwa na wafanyakazi kupitia mradi wa Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ)  jana.

  Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma, Dr, Laurent Ndumbaro (kulia) akimkabidhi Katibu Tawala Msaidizi na Rasilimali watu, Bernard Messelini, kifaa maalumu cha kutolea matangazo kwa wagonjwa na wafanyakazi  kupitia Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) makabidhiano yaliyofanyika jana.

No comments:

Post a Comment