Thursday, April 28, 2016

JIPU JENGINE LATUMBULIWA

NEWS: Maamuzi ya Rais Magufuli kwa Mkurugenzi mwingine leo April 28 2016

Taarifa ambayo imetoka April 28 2016 ni kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha Uwekezaji ‘TIC’, Julieth Kairuki kuanzia April 24 2016.
Hatua hii imechukuliwa baada ya Rais Magufuli kupata taarifa kwamba Mkurugenzi huyo hajachukua mshahara wa Serikali tangu alipoajiriwa mwezi April 2013 mpaka sasa, jambo ambalo linazua maswali mengi.
Taarifa hiyo iliyotolewa imesema endapo atakuwa tayari kufanya kazi na Serikali atapangiwa kazi nyingine na Clifford Katondo Tandari atakaimu nafasi ya Mkurugenzi Mtendaji.
utenguzi
CHANZO, millardayo

No comments:

Post a Comment