Saturday, April 30, 2016

SIO BAHARI, NI MAJI YALIYOZINGIRA NYUMBA ZAIDI YA 70 TANGA



 Wakazi wa Magaoni Tanga wakiangalia athari ya mafuriko baada ya mvua kubwa kunyesha kwa masaa 24 na kulazimika kaya zaidi ya 70 kuhamia shule ya msingi ya magaoni.
Kata ya Magaoni kwa miaka mingi imekuwa wahanga wa mafriko na wadau wa mazingira wamedai kuwa maji hayo yaliyozizingira nyumba sio mafuriko bali hayana miundombinu ya kupita.
Wamedai kuwa kila vipindi vya mvua eneo hilo hutuwaa maji kwa vile hayana pa kwenda hivyo kuomba halmashauri ya mipango miji kuchukua hatua za kuchimba mifereji ya kupita maji na kukomesha hofu kwa wakazi wa eno hilo.





No comments:

Post a Comment