Monday, January 16, 2017

UENDESHAJI PIKIPIKI BILA KUVAA KOFIA NGUMU (HELMENT) BODABODA MISHKAKI

 Uendeshaji wa vyombo vya moto bila kufuata sheria barabarani imekuwa ada kwa baadhi ya madereva jambo ambalo limekuwa likiongeza idadi ya ajali na vifo visababishwavyo na madereva hao.
Licha ya kikosi cha usalama barabarani kuongeza nguvu ya kudhibiti hali hiyo lakini baadhi ya madereva wanadaiwa kuwa wagumu wa kujua wajibu wao na sheria kw ajumla.
Kwa Mkoa wa Tanga kikosi cha usalama barabarni kimekuwa mwiba na kufanikiwa kudhibiti madereva wazembe wakiwemo ambao hawavai kofia ngumu hali ambayo ni nadra vifo visababishwavyo na pikipiki zaidi ya majeruhi.




Mwendesha pikipiki maarufu bodaboda akiwa amewapakiza wanafunzi watatu kuelekea shule ya msingi  Bombo Tanga ambao hawana kofia ngumu na kuhatarisha usalama wao

No comments:

Post a Comment