Thursday, January 19, 2017

JENGO REFU TEHRAN LAPOROMOKA

Jengo kubwa laporomoka Iran na kuua wengi

Hakuna kilichobaki wakati jengo hilo la ghorofa 17 lilipoporomoka
Wazima moto walikuwa wamepambana na moto huo kwa saa kadhaWazima moto wengi wanahofiwa kufa   baada ya jengo moja kubwa kwenye mji mkuu wa Iran Tehran, kushika moto na kuporomoka.
Wazima moto 200 walikabiliana na moto huo kwenye jengo hilo la ghorofa 17 kwa saa kadha, kabla ya kuporomoka kwa sekunde chache.
Zaidi ya watu 200 pia nao waliripotiwa kujeruhiwa kwenye mkasa huo.
Magari kumi ya kuzima moto yalifika eneo hilo na vituo vya runinga viliripoti kuwa wazima moto kadha walikuwa ndani ya jengo wakati liliporomoka.
Kituo kimoja cha runinga cha serikali kilinukuu afisa mmoja akisema kuwa kati ya watu 50 na 100 wanaaminiwa kukwama chini ya vifusi.
BBC

No comments:

Post a Comment