Jengo kubwa laporomoka Iran na kuua wengi

Wazima moto wengi wanahofiwa kufa baada ya jengo moja kubwa kwenye mji mkuu wa Iran Tehran, kushika moto na kuporomoka.Zaidi ya watu 200 pia nao waliripotiwa kujeruhiwa kwenye mkasa huo.
Magari kumi ya kuzima moto yalifika eneo hilo na vituo vya runinga viliripoti kuwa wazima moto kadha walikuwa ndani ya jengo wakati liliporomoka.
Kituo kimoja cha runinga cha serikali kilinukuu afisa mmoja akisema kuwa kati ya watu 50 na 100 wanaaminiwa kukwama chini ya vifusi.
BBC
No comments:
Post a Comment