Wednesday, January 25, 2017

MAREKANI KUJENGA UKUTA NA MEXICO

 Tutajenga ukuta katika mpaka na Mexico

Rais Donald Trump wa Marekani na mkewe Melanie
Ukuta utakaojengwa katika mpaka wa Marekani na MexicoRais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa siku kuu kuhusu usalama wa Marekani imepangwa ikiwemo tangazo la kujenga ukuta kati ya Marekani na Mexico.
Donald Trump amesema kuwa ujenzi wa ukuta mrefu wa wenye maili 2000 katika mpaka wa Mexico ni miongoni mwa mapendekezo yake wakati wa kampeni za urais.
Kutakuwa na mikakati ambayo pia italazimu miji mitakatifu nchini Marekani kushirikiana na mamlaka katika kuwarejesha makwao wahamiaji haramu.
Miji mitakatifu ni maeneo ambayo hayawakamati ama kuwazuilia wahamiaji wanaoishi katika taifa hilo kinyume na sheria.
BBC

No comments:

Post a Comment