Sunday, January 22, 2017

DIEGO COASTA ATABAKI DARAJANI, CONTE

Diego Costa anataka kusalia Chelsea

Diego Costa and Antonio Conte
Diego Costa anataka kuendelea kusalia Chelsea na ni miongoni mwa wachezaji walio tayari kucheza mechi ya Ligi Kuu ya Engand dhidi ya Hull Jumapili Leo , meneja Antonio Conte amesema.
Costa, 28, aliacha nje ya kikosi kilichoshinda mechi ya wikendi iliyopita dhidi ya Leicester baada yake kuzozana na mmoja wa wakufunzi kuhusu hali yake.
Hayo yalijiri huku kukiwa na uvumi kwamba alikuwa anatafutwa na klabu za Uchina.
Chelsea walisema aliachwa nje kutokana na maumivu ya mgongo, na kwamba alikuwa amefanya mazoezi pekee kwa siku mbili kama sehemu ya juhudi za kumsaidia kupata nafuu.

No comments:

Post a Comment