Tuesday, January 17, 2017

INDIA NA MPANGO KABAMBE WA KUTOKOMEZA UNYANYASAJI WA KIJINSIA WANAWAKE

Viti maalum kwenye ndege kuzuia unyanyasaji wa wanawake

Ndege ya abiria
Kampuni ya ndege ya Air India imeanza kuuza tiketi za ndege za viti vilivyotengewa wanawake pekee.
Viti sita vya mstari wa mbele katika ndege za abiria wa kipato cha wastani au 'economy' vimetengewa wanawake kufuatia ripoti za abiria wengine kuwanyanyasa baadhi ya wanawake.
Mkurugenzi mkuu kutoka kampuni hiyo ameliambia gazeti la The Hindu - kwamba wanataka kuwahakikishia abiria wanaosafiri peke yao.
Meenakshi Malik alisema: "kama kampuni kuu ya ndege nchini tunahisi ni jukumu letu kuhakikisha kuwa abiria wanawake wanasafiri kwa starehe."
Ndege hiyo pia sasa itasafiri ikiwa na maafisa wawili walinzi watakaokabiliana na abiria wasumbufu wasioweza kudhibitiwa.
Kuanzia baadaye wiki hii, iti hivyo sita vitauzwa katika ndege za Airbus A320 kwa safari za ndani nchini India.

No comments:

Post a Comment