Monday, January 23, 2017

KIMBUNGA CHAUA WATU 18 MAREKANI

Kimbunga Marekani: Watu 18 wauawa Georgia na Mississippi

MississippiVifusi Adel, Georgia, U.S. Januari 22, 2017Watu zaidi ya 18 wamefariki kutokana na kimbunga kikali na hali mbaya ya hewa kusini mwa Marekani, maafisa wa uokoaji wamesema.
Watu wengi wamejeruhiwa. Maeneo yaliyoathiriwa zaidi ni majimbo ya Georgia na Mississippi.
Gavana wa Nathan Deal ametangaza hali ya tahadhari katika wilaya saba kusini na katikati mwa Georgia ambapo watu 14 wamefariki.
Watu wanne waliuawa na vimbunga Mississippi siku ya Jumamosi.
Bado kuna hatari ya kimbunga kupiga maeneo ya kusini mwa Florida, idara ya taifa ya hali ya hewa imeonya.
Idara ya huduma za dharura ya Georgia imesema watu 14 walifariki katika wilaya za Cook, Brooks, Dougherty na Berrien katika jimbo la Georgia.

No comments:

Post a Comment