Monday, January 30, 2017

MNIGERIA ALIEDAIW AKUWA NA WAKE 86 AFARIKI DUNIA

Mohammed Bello Abubakar huenda alikuwa na zaidi ya wake 1Mhubiri mmoja wa zamani wa Kiislamu nchini Nigeria ambaye anadaiwa  alikuwa na takriban wanawake 86 ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 93.
Mohammed Bello Abubakar alifariki nyumbani kwake katika jimbo la Niger siku ya Jumamosi, kutokana na ugonjwa ambao haukutajwa
Watu wengi walihudhuria mazishi yake siku ya Jumapili.
Gazeti la Nigeria la Daily Trust liliripoti kuwa alipokuwa na wake 86 mwaka 2008 wakati aliangaziwa na vyombo vya habari, idadi hiyo inadaiwa ilipanda hadi wake 130 wakati wa kifo chake.
BBC

No comments:

Post a Comment