Friday, January 13, 2017

MVUTANO W AVISIWA UCHINA WAINGIA SURA MPYA NA MAREKANI

China yaionya Marekani kuhusu visiwa vinavyozozaniwa

Visiwa vilivyo katika bahari ya kusini mwa China
Kuizuia China katika kisiwa ilichojenga katika maji yanayogombaniwa huenda kukasababisha mvutano mkubwa, kituo cha habari cha serikali ya China kimsema.
Majibu hayo ya hasira yanajiri baada ya waziri mteule wa maswala ya kigeni nchini Marekani Rex Tillerson kusema kuwa Marekani inapaswa kuizuia Beijing kuingia katika visiwa vipya katika bahari ya kusini mwa China. .
Jarida la Global Times limeonya kwamba hatua kama hiyo inaweza kusababisha vita vikubwa.
Beijing imekuwa ikitengeneza visiwa katika miamba ya maji yanayogombaniwa na mataifa mengine.
Picha zilizochapishwa mwaka uliopita zinaonyesha ulinzi mkali katika baadhi ya visiwa hivyo.
BBC

No comments:

Post a Comment