Tuesday, January 31, 2017

WASAFIRI WA PEMBA HADI TANGA KUMEKUCHA



Tanga, KILIO cha muda mrefu cha wakazi wa Pemba na Tanga cha usafiri wa majini kimepata muarobani baada ya kampuni ya usafirishaji abiria na mizigo ya Azam Sealink 2, kuanzisha safari yake kwa mara ya kwanza juzi.
Usafiri huo utakuwa chachu kwa abiria na wafanyabiashara wa Tanga na Zanzibar ambao awali walikuwa wakitumia usafiri ambao sio salama na baadhi ya nyakati kutokea maafa na mizigo  kuzama baharini .
Akizungumza na waandishi wa habari, meneja wa meli hiyo ya  Azam Marinelink2, Hussein Said, amesema kilio cha Wanzanzibar hususani wakazi wa Pemba na Tanga wakiwemo wafanyabiashara kilikuwa kinawasononesha.
Alisema meli iko na uwezo wa kuchukua watu zaidi ya 2,000 waliokaa katika viti na shehena ya  mizigo pamoja na ubebaji wa magari.
“Kwa muda mrefu kilio cha wafanyabiashara na wasafiri kwa upande wa Tanga na Pemba tulikuwa tunajua ila muda muafaka ulikuwa bado, leo hii niseme kuwa muarobaini wake umepatikana” alisema Said na kuongeza
“Ujio huu wa meli utafufua uchumu na  biashara kwa pande zote mbili na Serikali kuongeza mapato yake hasa kuelekea ujengaji wa bomba la mafuta ambapo kuna fursa nyingi” alisema
Kwa upande wake mmoja wa wasafiri hao kutoka Pemba aliewasili kwa mara ya kwanza kwa kutumia meli hiyo, Ali Makame, amesema meli hiyo itakuwa mkombozi wa watu wa Pemba waishio Tanga na wafanyabiashara wa Tanga Pemba.
Alisema awali walikuwa wakitumia usafiri wa mashua ambao sio rasmi na baadhi ya nyakai kulazimika kupitia Unguja hadi Dar es Salaam ambako hutumia gharama kubwa.
“Ujio wa usafiri huu niseme kuwa ni mapinduzi makubwa kwa wasafiri wa majini kati ya Tanga na Pembao ambao tulikuwa tunahatarisha uhai wetu mikononi” alisema Makame
Aliyataka makampuni mengine kujitokeza hasa kipindi hiki cha ujio wa bomba la mafuta ambapo wafanyabiashara na wawekezaji wataweza kufika na kuangalia fursa za uwekezaji Tanga.
                                        















 Abiria kutoka kisiwani Pemba wakishuka kwenye meli ya Azama Sealink2 iliyotia nanga kwa mara ya kwanza katika bandari ya Tanga juzi.


 Moja ya vyumba vya VIP na viti vyake katika muonekano wake.

 Life Jarket zikiwa zimehifadhiwa  katika moja ya vyumba katika meli hiyo

No comments:

Post a Comment