Wednesday, September 23, 2015

ATAKAE VUNJA SHERIA KULA SIKUKUU KOROKORONI



Tangakumekuchablog
Tanga,JESHI la Polisi  Mkoani Tanga limesema  limejipanga kuhakikisha wananchi wanasherehekea Sikukuu ya Idd El Hajj kwa amani na utulivu na kutoa ovyo kwa madereva wa vyombo vya moto kuzingatia sheria.
Akizungumza na waandishi wa habari, ofisini kwake jioni hii, Kamanda wa polisi Mkoani Tanga, Zuberi Mombeji, alisema polisi itazidisha doria siku zote za Sikukuu kwa kutumia askari wa miguu wanaotumia mbwa na farassi pamoja na wa pikipiki.
Alisema itafanya doria katika maeneo ambayo ni korofi yanayotambulika kwa uporaji na wizi hivyo kuwahakikishia wananchi kuondoa hofu na kuwataka wazazi kuwa makini na watoto wao wakati wa matembezi.
“Sisi polisi niseme kuwa tumejipanga vilivyo na kuwahakikishia wananchi kusherehekea Idd kwa amani na utulivu----tuko na vikosi vya askari wanaotumia mbwa na farasi na wale wa pikipiki kazi yao ni kupita chochoroni kwa doria” alisema Mombeji na kuongeza
“Lakini niwaase marafiki zangu wa bodaboda kuwa mimi mwenyewe nitaongoza usalama barabarani ----bodaboda yeyote au dereva wa gari ataevunja sheria sikukuu ataililia korokoroni” alisema
Aliwataka madereva hao kuepuka kutumia vilevi na kuendesha vyombo vyao jambo ambalo amesema hatumvumilia mtu yoyote na sheria itatumika bila huruma na hivyo kuwaasa kuwa makini.
Kwa upande wa wazazi, kamanda Mombeji aliwataka kuwapa watoto wao wakati wa matembezi  watu wenye uelewa ikiwa lengo ni kuepuka kupotea pamoja na usalama wakati wakiwa katika matembezi barabarani.
Alisema vipindi vya sikukuu hujitokeza upotevu wa watoto jambo ambalo linasababishwa na wazazi kuwaruhusu watoto wao kufuatana na watu ambao hawajitambui.
Alisema jambo hilo limekuwa kero na kusababisha vipindio hivyo vya sikukuu wazazi na walezi kujazana katika vituo vya polisi kulizia watoto wao na hivyo kutaka lisijitokeze tena.
“Niwaombe wazazi kwanza kuwa makini na nyumba zao kwani wadokozi huutumia mwanya huo kwa kufanya udokozi----na ikumbukwe kuwaruhusu watoto wenu kwa kuongozana na watu wenye kujitambua” alisema Mombeji
Akitoa mkono wake wa Idd kwa wakazi wa Tanga, kamanda aliwatakia Sikukuu ya furaha na amani na kusema kuwa furaha hiyo iwe mwanzo mzuri wa kuelekea uchaguzi mkuu usikuwa na matukio ya uvunjifu wa amani.
                                                 Mwisho



No comments:

Post a Comment