Wednesday, September 23, 2015

MWALIMU AINGIA MATATANI NA MWANAFUNZI WAKE

Baada ya kuingia katika mahusiano ya kimapenzi na mwanafunzi wake mwalimu kakumbana na adhabu hii..


Nchi nyingi duniani kote ikiwemo Tanzania sheria ya mtu kuvuka umri wa kuitwa mtoto, hadi afikishe umri wa miaka 18 na kuendelea ndio inaaminika kuwa ni mtu mzima, ila mtu aliye chini ya miaka 18 haruhusiwi kutumia vitu kadhaa kama pombe, kujihusisha katika mahusiano ya kimapenzi hususani na mtu aliyemzidi umri.
JS72888632
Caroline Berriman
Licha ya kukiri kufanya kosa la kutembea na mwanafunzi wake mwalimu Caroline Berriman amehukumiwa kwenda jela. Caroline Berriman ambaye alikuwa ni mwalimu wa darasa msaidizi katika shule ya Abraham Moss Community, alishitakiwa kwa kosa la kufanya mapenzi na mwanafunzi wake aliye na umri wa miaka 16.
abraham-moss-school
Caroline Berriman ambaye ana umri wa miaka 30 kwa sasa, alishitakiwa kwa makosa mawili ya kufanya mapenzi na mtoto na kutenda kosa hilo katika sehemu inayoaminiwa na watu.
Caroline Berriman ambaye alikuwa mwalimu katika shule ya Abraham Moss Community iliyoko jijini Manchester, shule ambayo ina wanafunzi 1600 wenye umri kuanzia miaka 5 hadi 16 wa shule ya msingi na sekondari, amehukumiwa kwenda jela miaka miwili, kufanya kazi za kijamii za bila malipo kwa muda wa masaa 250 pamoja na kulipa pound 100 kama fidia kwa muhanga.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment