Wednesday, September 23, 2015

UBEBAJI VYUMA WAMPELEKA KABURINI

Mazoezi ya kunyanyua vyuma yapelekea kifo cha kijana huyu baada ya moyo wake kupasuka…

Imekuwa kawaida kwa vijana wengi siku hizi kupenda kunyanyua vyuma ili kujenga mwili wenye misuli mikubwa na muonekano mzuri. Utamaduni wa kubeba vitu vizito ili kujenga mwili wenye muonekano flani wa kuvutia unazidi kushika kasi duniani kote licha ya vijana wengi Tanzania wameonekana kuanza kufanya mazoezi ya kubeba vyuma kwa miaka ya hivi karibuni.
2CABB51200000578-0-image-a-11_1443007658948
Stori kutoka mtandao wa dailymail.co.uk umeripoti kifo cha Andrej Gajdos kijana mwenye umri wa miaka 19 na urefu wa futi 7 na inch 2, amefariki baada ya kubeba chuma na kupelekea misuli ya aorta katika moyo wake kupasuka. Andrej Gajdos alikuwa anaingia Gym mara mbili kwa siku na lengo lake lilikuwa kutengeneza mwili wake kuwa kama Dwayne Johnson.
2CAB8AD000000578-3245982-image-a-6_1443007639231
Dr John Oxley ndio aliufanyia uchunguzi mwili wa Andrej Gajdos na kuthibitisha moyo wa Andrej Gajdos kuwa na uzito usio wa kawaida wa gram 680 wakati binadamu wa kawaida moyo wake unatakiwa kuwa na uzito wa gram 400 hadi gram 500, hata hivyo uchunguzi bado umeeleza Andrej Gajdos kuwa na matatizo ya mapafu kwani njia ya kupitisha hewa katika mapafu yake imetanuka. Andrej Gajdos ni raia wa Slovakia amekutwa na umauti akiwa Tesco Uingereza.
2CAB8ABB00000578-3245982-image-a-17_1443000595637
2CAB8AC200000578-3245982-Andrej_Gajdos_19_died_suddenly_of_a_ruptured_aorta_the_main_arte-a-10_1443007658947
2CAB8C8500000578-3245982-He_had_aspirations_to_become_the_next_Rock_a_memorial_page_set_u-a-5_1443007639230
Dwayne Johnson.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment