Saturday, September 26, 2015

BASI LA TASHRIF LAPINDUKA NA DEREVA KUFARIKI HAPO HAPO



Tangakumekuchablog
Tanga, JESHI la Polisi Mkoani Tanga linamshikilia Mkandarasi mkazi wa Bombo Tanga, Endrew Kimunga (54) kwa tuhuma za kusababisha ajali iliyopelekea kupinduka basi la kampuni la Tashrif na dereva wake kufa papo hapo.
Tukio hilo lililotokea leo asubuhi eneo la Kange nje kidogo ya jiji la Tanga baada ya dereva wa gari aina ya Nissan Wagon, Kimunge kutoka kituo cha kuweka Petrol na kuingia barabarani kizembe jambo lililosababisha basi la Tashrif kushindwa kulikwepa na kuingia katika korongo na kupinduka.
Basi hilo ambalo lilikuwa likielekea kituo kikuu cha Mabasi yaendayo Mikoani cha Kange na kuelekea Dodoma lilipinduka baada ya dereva wake kushindwa kulikwepa jambo ambalo alilisukuma katika korongo na kupinduka .
Akizungumza na Tangakumekuchablog, Kamanda wa Polisi Mkoani Tanga, Zubery Mombeji, alisema tukio hilo lilitokea saa 12 ; 15 asubuhi eneo la Kange na kupeleka Dereva  wa basi, Mohammed Ayoub  kufa papo hapo  na kusababisha majeruhi wanne.
Alisema uchunguzi wa awali unaonyesha dereva wa Nissan Wagon, alishindwa kuzingatia sheria za barabarani na kusababisha uzembe baada ya kuingia barabara kuu bila kuangalia magari pande zote mbili.
“Uchunguzi wa awali unaonyesha dereva wa gari ndogo ndie chanzo cha ajali----kwa sasa tunaendelea na uchunguzi na tunamshikilia kwa mahojiano zaidi ya tukio zima” alisema Mombeji na kuongeza
“Dereva wa basi hakuwa na makosa ila ni kuwa amefariki pale pale----lakini niseme kuwa bado tuko katika uchunguzi na dereva wa Nissan tunamshikilia kituo kikuu cha Chumbageni” alisema
Aliwataja majeruhi kuwa ni Twaha Juma(42) mkazi wa Msambweni  pamoja na Idd Omary  ambao wote ni wafanyakazi wa kampuni ya Tashrif
Akizungumzia tukio zima la ajali hiyo, Kamanda Mombeji, alisema Dereva wa basi hilo la Tashrif , Mohammed Ayoub, hakufunga mkanda na kuwa chanzo cha kifo chake baada ya kurushwa mbele ya kioo cha mbele na gari kumkokota na kupelekea kusagwasagwa.
Alisema kama angelifunga mkanda angelisalimika kifo kama ilivyokuwa kwa wenzake wawili ambao walikuwa siti za katikati na kupelekea kupata majeraha madogo madogo.
                                                     Mwisho







No comments:

Post a Comment