Tuesday, September 22, 2015

MASIKINI " MAJONZI

Mapenzi yanaumiza na wengine wanashindwa kuyahimili maumivu.

NTVNi binti Wanjiru Kamanda wa miaka 21 tu ndio amefanya mpaka nimeiandika hii taarifa hapa, alikua mapenzini na kijana Farid Mohammed (24) lakini sasa hivi mapenzi yao yamekuwa habari nyingine.
Kilichotokea kwa wawili hawa huko Buruburu Kenya ni kwamba msg ya mapenzi ya Mwanamke mwingine ilikutwa kwenye simu ya boyfriend ambaye ni Farid, Wanjiku akashindwa kujizuia na kumchoma kwa kitu chenye ncha kali zaidi ya 20 mgongoni, tumboni, kifuani na kwenye shingo.
Pamoja na Farid kupelekwa Hospitali Madaktari hawakuweza kuokoa maisha yake na kwa sasa Wanjiru amelazwa kwenye Hospitali ya Kenyatta Nairobi Kenya akiwa na pingu kwenye kitanda chake huku Polisi wakiendelea na uchunguzi.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment