Wednesday, September 23, 2015

UBIZE WA KUITUMIKIA KLABU , ARSENAL WENGER, MKE AKIMBIA

Baada ya stori nyingi kuhusu Ndoa ya Arsene Wenger kuvunjika, haya mengine yameandikwa leo

Baada ya zile tetesi za muda mrefu kuhusiana na kocha wa klabu ya Arsenal Arsene Wenger kutokuwa na maelewano mazuri na mkewe Annie, stori kutoka mtandao wa mirror.co.uk umethibitisha kutengana kwao, awali kulikuwa na uvumi wa wanandoa hao kuachana kutokana na kutoonekana wakiwa katika picha ya pamoja toka mwaka 2013.
article-2451933-189E015E00000578-726_634x699
Picha hii walipiga pamoja October 2013
Stori kutoka mtandao wa mirror.co.uk September 23 unaeleza wawili hao kutengana na kukubaliana kisheria kugawana baadhi ya mali na fedha, kikubwa kinachotajwa kuharibu mahusiano yao ni ubize wa Arsene Wenger katika klabu yake ya Arsenal. Wenger mwenye umri wa miaka 65 na mkewe Annie mwenye umri wa miaka 59 hawakuwa pamoja toka mwezi June mwaka huu.
Arsene-Wenger-and-wife-split (2)
Wenger na mkewe Annie walifunga ndoa December 2010 baada ya kuwa katika mahusiano ya muda mrefu na wamefanikiwa kumpata mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 18. Nyaraka ya kisheria ya kifaransa  “séparé du corps” haimaanishi kuwa Wenger na Annie wameachana kwa talaka ila haiwaruhusu kuishi pamoja.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment