Wednesday, September 23, 2015

MAISHA NI SAFARI NDEFU

Hawa mastaa nao wamepitia magumu sana, wengine walifungwa mpaka Gerezani..

Maisha ya Mastaa Behind the Scenes kuna vitu vingi sana huwa nje havijulikani, lakini ukiangalia tu kwamba wao ni binadamu basi ni lazima kuna time wanakutana na mambo magumu na wakati mwingine mambo ni poa kama tu inavyotokea kwa mtu mwingine!
Nimeikuta hii story kwenye zile ambazo zimeandikwa pia kwenye kurasa zinazohusu maisha ya Mastaa mtaani, yani kwenye maisha yao nje ya sanaa wanazofanya mbele ya Camera.. wengine story zao zinasikitisha sana ikiwemo kujihusisha na dawa za kulevya, matukio ya silaha na wapo waliowahi kufungwa pia.
1. Michael Gerard “Mike” Tyson
mike-tyson-pic-getty-image-1-266516999
Mike Tyson, moja ya Mabondia ambao wameacha kumbukumbu za Rekodi kubwa kwenye Boxing miaka ya nyuma kabla ya kustaafu mwaka 2006.
Mwaka 1991 Mike Tyson alikamatwa kwa kesi ya kubaka, japo  mwenyewe alidai kwamba hakufanya kitendo hicho ila iikuwa makubaliano ya wao wawili, yani Mike mwenyewe na Mrembo Young Desiree Washington ambaye alikuwa na umri wa miaka 18 wakati huo.
iron-mike-tyson-617141460
Hapo ni Mike Tyson enzi hizo akiwa kwenye Ulingo wa Boxing kuusaka Ubingwa.
Mwaka 1992 alifungwa kifungo cha miaka sita jela lakini aliachiwa baada ya kutumikia kifungo kwa miaka miwili, baadae mwaka 1999 Mike alirudi tena Jela kutumikia kifungo cha miezi tisa jela baada ya kujeruhi watu wawili kwenye ajali ya barabarani ambayo aliisababisha.
2007-jail_1410942i
Mike alikamatwa tena mwaka 2007, alikuwa akiendesha gari huku amelewa, akakaa jela siku moja alafu akafungwa kifungo cha nje kwa miaka mitatu akiwa chini ya uangalizi maalum.
2. Robert Downey Jr
Robert Downey Jr
Robert Downey Jr jamaa ni moja ya mastaa wa movie Hollywood, kwenye zile kali alizowahi kufanya, ziko pia movie za ‘The Avengers’ na ‘Iron Man’.
Robert Downey Jr alifundishwa kutumia Dawa za kulevya na baba yake akiwa na umri wa miaka 8.. kwenye Kesi alizowahi kukutana nazo iko pia ya kukamatwa akiwa anaendesha gari kwa speed kubwa huku akiwa na dawa za kulevya, Heroine, Cocaine pamoja na bunduki. Kuna wakati alilewa dawa za kulevya kiasi cha kujikuta akipotea na kuingia kwenye nyumba ya jirani yake ambaye alikuwa amelala wakati wa usiku.
Iron-Man_wallpapers_274
Robert Downey Jr kwenye movie ya ‘Iron Man’.
Robert alifungwa kwa miaka mitatu kifungo cha nje lakini akakiuka masharti ikiwemo la kutotumia dawa za kulevya, akakamatwa na kufungwa jela miezi sita… jamaa aliachiwa mwaka 1999 lakini akakamatwa tena baada ya kukiuka sharti la kwenda kupimwa kama anatumia dawa za kulevya, akakaa Jela mwaka mmoja, alipoachiwa akaona abadili maisha yake kwa kujiweka busy zaidi na kucheza movie.
 3. Wesley Snipes
Wesley-Snipes-in-Blade-02
Wesley Snipes ni mkali sana wa action movies toka Hollywood Marekani, aliwahi kucheza pia kwenye movie ya ‘Blade’ pamoja na ‘The Expendables 3’ pamoja na wakali wengine ikiwemo akina Jason Statham.
Wesley Snipes kuna wakati alijikuta akiingia kwenye Milango ya Magereza na kutumikia kifungo cha miaka mitatu kwa kosa la kukwepa Kodi.
Jamaa alianza kutumikia kifungo kuanzia mwaka 2000 mpaka 2013, alipotoka akarudi kazini kwa kushiriki kwenye Movie ya The Expendables 3 japo aliendelea kulalamika kwamba mbona wakwepa Kodi wako wengi lakini akakamatwa pekeyake ?!
4. Curtis James Jackson III aka 50 Cent
LAS VEGAS, NV - JUNE 01: Boxer Floyd Maywether Jr. arrives at the Clark County Regional Justice Center accompanied by Curtis ''50 Cent'' Jackson as he surrenders to serve a three-month jail sentence at the Clark County Detention CenterÊon June 1, 2012 in Las Vegas, Nevada. Mayweather pleaded guilty in December to attacking his ex-girlfriend while two of their children watched in September 2010. (Photo by David Becker/Getty Images)
Rapper 50 Cent.
Kama umepata nafasi ya kucheki movie ya jamaa ya Get Rich or Die Tryin’, anasema hiyo movie imezungumia sehemu kubwa sana maisha yake kuanzia alikotoka mpaka alipofika sasahivi, maisha yalikuwa magumu ikafanya awe karibu sana na matukio ya uhalifu tena wakati akiwa na umri mdogo.
Get Rich
Kama hujui taarifa ikufikie kwamba 50 Cent alianza kuuza Dawa za kulevya akiwa na umri wa miaka 12 tu, 50 Cent aliwahi kupigwa risasi tisa akiwa kwenye mazingira ya biashara ya Dawa za kulevya, baadaye mwaka 1994 alikamatwa na Polisi kwa kosa la kukutwa na cocaine, heroine na Bastola nyumbani kwao…
Alihukumiwa kifungo kati ya miaka mitatu mpaka tisa jela lakini baadaye aliachiwa huru na kuamua kujihusisha na biashara safi ikiwemo kuingia kwenye muziki.
5. Ja Rule
Ja Rule
Jeffrey Atkins aka Ja Rule ni Rapper mkubwa sana na mwenye sauti ya pekeyake, hajasikika kwa muda mrefu sana ila jina lake bado wale fans wa muziki wake bado wanamkumbuka.
Sio stori ngeni kwa marapper wa Marekani kuingia kwenye matatizo na Sheria za nchi yao… Ja Rule nae amewahi kujikuta kwenye vitanzi mara kadhaa hivi na kusomewa hukumu kwenda jela.
Ja-Rule-Fresh-Out-Da-Pen
Ukiachana na ishu ya kukamatwa akiwa na Bangi na kuendesha gari huku akiwa na leseni iliyokwisha muda wake, mwaka 2007 aliingia kwenye noma nyingine akiwa na rapper Lil Wayne, jamaa alikutwa na Bastola pamoja na Dawa za kulevya, akaenda jela miaka miwili kuanzia mwaka 2010… haukupita muda mrefu akakutwa na hatia ya kukwepa kodi, akaendelea kutumikia kifungo mpaka mwaka 2013.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment